0715 72 92 92

SHABAN KALUSE

Kwa Matangazo na mambo mbalimbali & Wasiliana Nami

http://www.serenahotels.com/serenadaressalaam/default-en.html

Nov 26, 2008

MTOTO WA MIEZI MINNE AZUNGUMZA MAZITO

Habari hii nimeidesa kutoka kwenye mtandao wa Jamii Forums.


Na Mashaka Mhando, Tanga


MTOTO wa miezi minne aliyezaliwa kwenye hospitali teule wilayani Muheza, amekuwa gumzo na kustaajabisha wakazi wa mji huo, wakiwamo wazazi wake, kutokana na kuzungumza akiwa na umri huo. Mtoto huyo pichani aliyezaliwa Julai 16 mwaka huu, licha ya kuzungumza, pia amekuwa kituko kutokana na kutaka aitwe majina matatu ya Glory, Halima na Upendo, pindi anapoitwa na mtu yeyote akitaka kumsalimia.

Akizungumza juzi kwenye ofisi za gazeti hili barabara ya 15 Jijini hapa, mama wa mtoto huyo Bi Rosemary Mhina, mkazi wa mtaa wa Bin Seif, wilayani Muheza, alidai kuwa mtoto wake huyo ni wa ajabu kwani tangu akiwa mjamzito wa miezi saba, alikuwa akilia tumboni. "Kwanza nilipokuwa na mimba, tumbo lilikuwa linaniuma sana, nilipofikisha miezi saba tumbo likiniuma, utamsikia mtoto analia tumboni, nikaenda hospitali, nilianzia Teule, nikaja huku Bombo na

Tumaini, nilipopigwa 'ultra-sound' madaktari wakanieleza kuwa nitajifungua mtoto wa kiume, waliyemwona tumboni kwa kifaa hicho," alisema Bi Rosemary. Akielezea zaidi kuhusu namna alivyobaini mtoto wake kuwa na mawasiliano na watu, mama huyo alidai kuwa mara baada ya kuzaliwa, alipofikisha miezi miwili, siku moja alilia sana wakati akimbembeleza "Nyamaza mwanangu usilie ngoja nikupewa maziwa".

Alisema baada ya kumweleza hivyo, mtoto huyo alitamka maneno yaliyomtisha mama yake huyo: "Mama usione nalia, nalizwa na mengi, kwanza baba alitaka uniue nikiwa tumboni, halafu maisha yako si mazuri mama nakuonea huruma." Bi Rosemary alikiri kwamba baada ya kupata ujauzito kutoka kwa mwanaume (jina tunalihifadhi) ambaye amedai kwamba anafanya kazi katika hospitali ya Mount Meru, Arusha, alimpa sh. 30,000 ili akaitoe hospitalini wakati mimba hiyo ilipofikisha miezi sita. "Yule baba alitaka nikatoe mimba ya mtoto huyu nikakataa, hata hivyo wazazi wangu hawakutaka mimi nizae baada ya kuwa na watoto wawili, niliogopa pengine ningefanya hivyo ungekuwa mwisho wangu," alidai Bi Rosemary.

Aliendelea kudai kuwa tangu mwanawe huyo awe naye amekuwa akitokewa na miujiza mingi na kipindi alichoanza kuzungumza, alimpeleka kwa wachungaji mbalimbali ili kumwombea, lakini kila anapokwenda huko akirudi anatokewa na vituko. "Kipindi kimoja nilimpeleka kuombewa, usiku niliona paka wengi ndani nilimolala wakaniparura huku mwanangu Upendo akinicheka," alidai. Mama huyo ameomba watu wamsaidie ili mtoto huyo asiwe na vituko hivyo kwani hivi sasa baba wa mtoto amemkimbia na hana mawasiliano naye tena.

HAKIKA DUNIANI KUNA MAMBO

No comments:
Andika Maoni Maoni

This Blog Designed by DonSoo, Contact 0656212326.DonSoo
Kaa Karibu na Mimi